Skip to main content

Tumia mbinu hii ili kupata majibu ya changamoto inayokukabili




Miasha ya mwanadamu yamejawa na changamoto na shida mbalimbali. Changamoto hizo hizo, wapo baadhi ya watu huzivumilia katika kutenda jambo fulani, lakini pia wapo baadhi ya watu hukta tamaa kabisa. Na hao ambao hukata tamaa ndio ile idadi kubwa ya watu ambao hufa na ndoto zao mapema.

Lakini ukweli ni kwamba changamoto na shinda mbalimbali za maisha ni kipimo cha akili, kwani wapo baadhi ya waimbaji wa nyimbo huimba katika nyimbo zao na kusema changamoto ni majaribu, na majribu ni mtaji. Hivyo katika maisha haya ni jambo la ajabu sana kama utaendelea kukataa tamaa kwa sababu ya changamoto Fulani.

Na ukweli ni kwamba ili uweze kufanikiwa wanasema changamoto hazikwepeki, na changamoto ndio njia ambayo itakufikisha kule ambapo unataka kufika, endapo tu utaamua kupambana na changamoto hizo.

Swali linakuja nawezaje kupambana na changamoto hizo?

Jambo la msingi unalotakiwa kufanya ni kuhakikisha unapambana na changamoto za maisha ni;

1. Orodhesha changamoto zote ambazo zinakukubali. Hata kama zipo zaidi ya changamoto tano ainisha zote.

2. Baada ya kuorodhesha changamoto hizo tano, jambo ambalo unatakiwa kufanya baada ya hapo unatakiwa kuchugua jambo ambalo lina umuhimu sana katika kulitekeleza.

3. Baada ya kulipata jambo hilo, usiishie kulichagua tu. Tafuta mbinu ya jinsi ya kuondokana na changamoto hiyo. Na mbinu hizo ziandikwe mahali ambapo panaonekana na uanze utekelezaji mara moja.

Mbinu hii ya kupambana na changamoto itakusaidia sana katika kupiga hatua mbele zaidi kivitendo kuliko kukata tamaa.

Nimekupa mbinu hii, kwa sababu wengi wengi huwa tunajitenga na chanagamoto za kimaisha hasa pale zinapojitokeza. Lakini kama nilivyoeleza hapo awali ni kwamba changamoto za kimaisha ni kigezo tosha cha kuweza kutimiza ndoto yako, jambo la msingi tafuta majibu ya jinsi ya kuondokana na changamoto hiyo.

Kama hutatafuta majibu ya changamoto zinazokukabli itakuwa ni sawa na bure, kwani utazidi kuwa maskini maisha yako yote.


Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>