Skip to main content

Tumia mbinu hii ili kupata majibu ya changamoto inayokukabili




Miasha ya mwanadamu yamejawa na changamoto na shida mbalimbali. Changamoto hizo hizo, wapo baadhi ya watu huzivumilia katika kutenda jambo fulani, lakini pia wapo baadhi ya watu hukta tamaa kabisa. Na hao ambao hukata tamaa ndio ile idadi kubwa ya watu ambao hufa na ndoto zao mapema.

Lakini ukweli ni kwamba changamoto na shinda mbalimbali za maisha ni kipimo cha akili, kwani wapo baadhi ya waimbaji wa nyimbo huimba katika nyimbo zao na kusema changamoto ni majaribu, na majribu ni mtaji. Hivyo katika maisha haya ni jambo la ajabu sana kama utaendelea kukataa tamaa kwa sababu ya changamoto Fulani.

Na ukweli ni kwamba ili uweze kufanikiwa wanasema changamoto hazikwepeki, na changamoto ndio njia ambayo itakufikisha kule ambapo unataka kufika, endapo tu utaamua kupambana na changamoto hizo.

Swali linakuja nawezaje kupambana na changamoto hizo?

Jambo la msingi unalotakiwa kufanya ni kuhakikisha unapambana na changamoto za maisha ni;

1. Orodhesha changamoto zote ambazo zinakukubali. Hata kama zipo zaidi ya changamoto tano ainisha zote.

2. Baada ya kuorodhesha changamoto hizo tano, jambo ambalo unatakiwa kufanya baada ya hapo unatakiwa kuchugua jambo ambalo lina umuhimu sana katika kulitekeleza.

3. Baada ya kulipata jambo hilo, usiishie kulichagua tu. Tafuta mbinu ya jinsi ya kuondokana na changamoto hiyo. Na mbinu hizo ziandikwe mahali ambapo panaonekana na uanze utekelezaji mara moja.

Mbinu hii ya kupambana na changamoto itakusaidia sana katika kupiga hatua mbele zaidi kivitendo kuliko kukata tamaa.

Nimekupa mbinu hii, kwa sababu wengi wengi huwa tunajitenga na chanagamoto za kimaisha hasa pale zinapojitokeza. Lakini kama nilivyoeleza hapo awali ni kwamba changamoto za kimaisha ni kigezo tosha cha kuweza kutimiza ndoto yako, jambo la msingi tafuta majibu ya jinsi ya kuondokana na changamoto hiyo.

Kama hutatafuta majibu ya changamoto zinazokukabli itakuwa ni sawa na bure, kwani utazidi kuwa maskini maisha yako yote.


Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).