Skip to main content

YAELEZWA MSONGO WA MAWAZO HUSABABISHA KUZAA MTOTO MLEMAVU WA AKILI




Msongo wa mawazo wakati wa ujauzito ni miongoni mwa sababu za kuzaa mtoto mwenye ulemavu wa akili.

Hayo yameelezwa na mtaalamu wa magonjwa ya akili, Mwanaidi Hamza katika kituo cha matibabu ya magonjwa hayo kilichopo Hospitali ya Rufaa ya Bombo mkoani Tanga.

Alisema msongo wa mawazo husababisha athari kwa mjamzito, lakini athari kubwa huenda kwa mtoto na wakati mwingine husababisha udumavu.

“Kwa sasa kuna kesi nyingi za watoto kushindwa kuendana na hatua za ukuaji wa watoto kunakotokana na athari za msongo wa mawazo,” alisema Mwanaidi.

Alisema unaweza kukuta mtoto ana miezi sita, lakini bado hata kunyanyua mkono hawezi.

“Hiyo inatokana na athari za msongo wa mawazo,” alisema Mwanaidi.

Alisema licha ya mihangaiko ya maisha, lazima jamii imwepushe mjamzito matatizo yatakayomsababishia msongo wa mawazo ili aweze kuzaa mtoto mwenye afya bora.

Mwanaidi alisema tatizo la kuzaa watoto wenye ulemavu linaweza kwisha kabisa kwenye jamii iwapo wazazi watazingatia lishe bora.

“Ni elimu pekee ndiyo itakayoweza kuleta mabadiliko kwa jamii na kuachana na mila potofu ambazo zimepitwa na wakati,” alisema.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.