Skip to main content

WADAU WA KILIMO WATOA USHAURI KWA SERIKALI



Na. Ezekiel Mtonyole, Chamwino

Serikali imeshauriwa kuwapa mfunzo ya mara kwa mara maafisa ugani ili kuwajengea uwezo wa kuwafundisha na kuwasaidia wakulima namna bora ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazotokana na mabadiliko ya mifumo ya kilimo hapa nchini.

Wakizungumza wakati wa maonyesho maalumu ya mbegu na vyakula asilia yaliyofanyika Wilayani Chamwino, Mkoani Dodoma, baadhi ya wakulima wadogo wadogo walisema changamoto hizo ni pamoja na mabadiliko ya tabia nchi, matumizi bora ya mbegu, mbolea pamoja na janga la uchakavu wa udongo.

Akiongea kwa niaba ya wakulima hao  Mwenyekiti wa   Jukwaa la Wakulima wadogo wilayani Chamwino  (JUWACHA)  Mkoani Dodoma  chini ya ufadhi wa Shrika lisilo la Kiserikali Action Aid Janeth Nyamayahasi amesema  Maofisa Ugani wanashindwa kutoa elimu ya kutosha pamoja na  matumizi bora ya ardhi na mbegu bora kutokana na ukosefu wa mafunzo ya  mara kwa mara.

"Kuna haja ya serikali kuona namna ya kuwapa elimu wataalamu wa kilimo, hasa kipindi hiki mabadiliko ya tabia ya nchi na kuwajengea uwezo wakulima namna ya kukabiliana na changamoto hiyo" amesema Janeth.

Akiendelea kufafanua amesema maofisa ugani wengi  wanashindwa kutekeleza  majukumu yao ipasavyo kwa madai yakukwamishwa madaraka kama  maafisa ardhi.

Hata hivyo amesema miongoni mwa Changamoto zinazowakabili wakulima ni pamoja na uhaba wa pembejeo na  zikipatikana zinachelewa kufika  kwa wakati, ukosefu wa masoko ya uhakika na uhaba pia wa maofisa ugani.

Licha ya hayo yote, amelipongeza Shirika la Action Aid kwa kuwa mstari wa mbele katika jitihada za kuwawezesha wakulima wanawake wadogowadogo vijijini kulima kwa kufuata kanuni za kitaalamu na kuwajendea uwezo wa kuweza kumiliki ardhi.

Kwa upande wake, Mratibu wa Shirika la PELUM Tanzania, Donati Senzia, amesema lengo la maonyesho  hayo ni kuhamasisha jamii juu ya matumizi ya chakula cha asili,kuhamasisha jamii kuendeleza mfumo wa mbegu za asili na kuwakutanisha wakulima na wataalamu wa mbegu.

Taasisi na mashirika mengine yaliyoshiriki katika maonesho hayo ni pamoja na  Wakala wa Mbegu Tanzania (ASA), Kituo cha Tafiti za Kilimo Tanzania (TARI), AGRA na  RIPAT.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.