Skip to main content

SWAHILI FASHION WEEK KUFANYIKA DECEMBER



Maonesho ya mavazi ya Swahili Fashion Week yanatarajiwa kufanyika Disemba Sita, Saba na Nane mwaka huu katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.

Maonesho hayo yanafanyika kwa mara ya 12 ambapo pia zitatolewa Tuzo katika vipengele 26, kwa ajili ya kutambua mchango wa Wadau mbalimbali kwenye tasnia ya ubunifu.

Pamoja na mambo mengine, wakati wa maonesho hayo ya mavazi ya Swahili Fashion Week kutakua na mauzo ya wazi ya mavazi mbalimbali.

Wabunifu 34 wa mavazi kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na katika Mataifa mengine Duniani, wataonyesha vipaji vyao wakati wa maonesho hayo.

Onesho la mavazi la Swahili Fashion Week, limekua likifanyika kila mwaka ambapo Wabunifu wa mitindo na Warembo kutoka nchi zinazozungumza lugha ya Kiswahili na nchi nyingine Duniani wanatumia fursa hiyo kuonyesha vipaji vyao pamoja na kuuza ubunifu wao.

Muasisi wa Swahili Fashion Week, - Mustafa Hassanali ametoa wito kwa Watanzania kupenda kuvaa mavazi yaliyobuniwa na Wabunifu wa Tanzania ili kukuza vipaji pamoja na vipato vyao.


Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>