Skip to main content

SWAHILI FASHION WEEK KUFANYIKA DECEMBER



Maonesho ya mavazi ya Swahili Fashion Week yanatarajiwa kufanyika Disemba Sita, Saba na Nane mwaka huu katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.

Maonesho hayo yanafanyika kwa mara ya 12 ambapo pia zitatolewa Tuzo katika vipengele 26, kwa ajili ya kutambua mchango wa Wadau mbalimbali kwenye tasnia ya ubunifu.

Pamoja na mambo mengine, wakati wa maonesho hayo ya mavazi ya Swahili Fashion Week kutakua na mauzo ya wazi ya mavazi mbalimbali.

Wabunifu 34 wa mavazi kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na katika Mataifa mengine Duniani, wataonyesha vipaji vyao wakati wa maonesho hayo.

Onesho la mavazi la Swahili Fashion Week, limekua likifanyika kila mwaka ambapo Wabunifu wa mitindo na Warembo kutoka nchi zinazozungumza lugha ya Kiswahili na nchi nyingine Duniani wanatumia fursa hiyo kuonyesha vipaji vyao pamoja na kuuza ubunifu wao.

Muasisi wa Swahili Fashion Week, - Mustafa Hassanali ametoa wito kwa Watanzania kupenda kuvaa mavazi yaliyobuniwa na Wabunifu wa Tanzania ili kukuza vipaji pamoja na vipato vyao.


Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).