Skip to main content

SERIKALI YAKIRI KUTOKUWA NA TAKWIMU ZA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA



Serikali nchini imekiri kutokuwa na takwimu nyingi za magonjwa yasioambukizwa na hivyo kuzitaka taasisi mbalimbali za tafiti kuhakikisha zinawekeza kwenye mambo ya utafiti wa magonjwa hayo.

Aidha katika kukabiliana na magonjwa hayo pia Serikali inatarajia kufanya uzinduzi wa mpango huo ili kukabiliana na hali hiyo Novemba 14, 2019 Jijini Dodoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa afya maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndungulile wakati akifungua kongamano la kisayansi lililowakutanisha wadau wa sekta mbalimbali wakiwemo wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Amesema kukosekana kwa takwimu nyingi za magonjwa yasiyoambukizwa imekuwa ni chanzo cha uwepo wa changamoto na hivyo kupelekea magonjwa hayo kuongezeka kwa kasi ikilinganishwa na kipindi cha nyuma.

“Hakikisheni mnawekeza kwenye tafiti ili kuufanya mpango huu kufanikiwa maana tusipokuwa na takwimu za kutosha huu mpango hautakuwa na maana tafiti za kimfumo zinatakiwa ili tujue ni kwa nini tunakuwa na theluthi moja ya watoto wenye utapiamlo nchini wakati tuna chakula cha kutosha,” amesisitiza Dkt. Ndungulile.

Hata hivyo amesema ipo changamoto katika matibatu ya magonjwa hayo kwani mwananchi wa kawaida amekuwa akishindwa kumudu gharama na kutaka kuwepo kwa habari itakayosaidia kukabiliana nayo ikiwa ni pamoja na ushiriki wao katika utekelezaji wa mpango wa Serikali.

Awali Mkurugenzi wa tiba Wizara ya afya maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na Watoto Dkt. Grace Magembe amesema tathimini ya hivi karibuni ya mpango mkakati wa sekta ya afya imegundua kuwa magonjwa yasiyoambukizwa yanachangia zaidi ya asilimia 30 ya vifo Kitaifa na asilimia 70 Kimataifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya Taifa ya utafiti wamagonjwa yabinadamu (NIMR), Yunus Mgaya amesema mzigo wa magojwa yasiyoambukiza ni mkubwa hali inayopelekea kuathiri maendeleo ya nchi kwani wanaosumbuliwa zaidi ni vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa.

“Tafiti mbalimbali zimekuwa zikifanyika juu ya magonjwa yasioambukizwa na imebainika kuwa magonjwa yasiyopewa kipaumbele yanachangia kuongezaka kwa vifo na mkutano huu utasaidia kuwa na kauli moja ya kuhakikisha tunapunguza magonjwa haya,” amesisitiza Mgaya.

Mfumuko wa bei wa Taifa wapanda
Hata hivyo amebainisha kuwa utoaji wa elimu kwa jamii una mafanikio zaidi na kwamba kuna ulazima wa kuweka mikakati juu ya nini kifanyike ili kupunguza idadi ya wagonjwa na jinsi ya kupambana na kujikinga nayo.

Akiongea katika kongamano hilo mmoja wa vijana wanaosumbuliwa na ugonjwa wa kisukari James Chumi amesema pia suala la imani za kishirikina zimekuwa zikichangia kwa watu wengi kuchelewa kufikishwa hospitalini kwa ajili ya kupata matibabu.

Kutokana na hali hiyo Chumi ameiomba Serikali pamoja na wadau wengine kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili kuwa na uelewa wa magonjwa hayo kwani wengi huathirika kwa kukosa msaada wa mapema.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.