Skip to main content

TANZANIA YAPUNGUZA UINGIZAJI WA DAWA ZA KULEVYA AINA YA HEROIN KWA ASILIMIA 90


Na,Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Kwa  mujibu wa Shirika la Kimataifa  la kupambana na dawa za kulevya na Uhalifu[UNODC],Tanzania ilipunguza uingizaji wa dawa za kulevya aina ya Heroin  kwa asilimia 90% .
 
Hayo yamesemwa  Nov.6,2019  na Waziri wan chi,Ofisi ya Waziri Mkuu ,Sera,Bunge ,kazi,vijana ,Ajira  na watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama wakati akizungumza na Waandishi wa Habari bungeni jijini Dodoma mara baada ya kuwasilisha  bungeni Taarifa ya Hali za Dawa za Kulevya  ya mwaka 2018.
 
Mhe.Mhagama amesema pamoja na jitihada zilizofanywa na serikali katika kupambana na dawa za kulevya ,bangi imeendelea kuwa tatizo hapa nchini ambapo ametaja mikoa ambayo imeonekana  kuathirika zaidi na kilimo cha bangi ni pamoja na Mara,Tanga,Morogoro,Arusha,Kagera na Ruvuma huku pia Mirungi ikiendelea kutumiwa na watu wa rika hapa nchini.
 
Aidha,Mhe.Mhagama amesema kwa kipindi cha mwaka 2018 juhudi ya vyombo vya dola kwa kushirikiana na wananchi zilifanikiwa ukamataji wa tani 24.3 za bangi zikiwahusisha watuhumiwa 10,061 na tani 8.97 za mirungi  zikiwahusisha watuhumiwa  1,186.
 
Katika kipindi cha Mwaka 2018 jumla ya kesi 7,593 zikiwa  na jumla ya watuhumiwa 10,979  zilifunguliwa katika mahakama mbalimbali nchini huku jumla ya kesi 7,174 zilizowahusisha watuhumiwa 11,045 ziliendelea   kusikilizwa.
 
Pia,Mhe.Mhagama amesema serikali imeendelea kutoa huduma  za tiba  kwa watumiaji wa dawa za kulevya  ambapo jumla ya vituo 6 vilivyopo katika mikoa ya  Dar Es Salaam,Mwanza,Mbeya,na Dodoma viliendelea kutoa huduma   na hadi kufikia mwaka 2018 ,zaidi ya watumiaji elfu nane[8000] waliendelea kupatiwa huduma za Methadone  katika vituo husika.
 
Hivyo,Waziri Mhagama ameendelea kufafanua serikali itaendelea kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya huku akivipongeza vyombo vya habari pamoja na wadau mbalimbali kwa kuendelea kusisitiza madhara ya dawa za kulevya kwa Taifa la Tanzania.

Kwa upande wake kamishna wa Kinga na tiba kutoka Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya  nchini Dokta Peter Mfisi amesema bei ya dawa ya kutibu waathirika wa dawa za kulevya [methadone] inanunuliwa kwa Soko la India kati ya dola 650 hadi dola 700 na kilo moja ya Methadone inawezakuhudumia watu 650 mpaka 700.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>