Skip to main content

NACTE YATANGAZA AWAMU YA NNE YA UDAHILI KATIKA NGAZI YA ASTASHAHADA NA STASHAHADA KWENYE VYUO NA TAASISI MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2019/2020


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linautangazia umma kwamba limefungua dirisha la udahili kwa AWAMU YA NNE na ya mwisho, kwenye Vyuo na Taasisi zinazotoa programu za Astashahada na Stashahada hapa nchini, zinazotambuliwa na Baraza kuanzia tarehe  1 Novemba, 2019  hadi tarehe 10 Novemba, 2019 ambapo dirisha hilo litafungwa.

Hatua hiyo imekuja kufuatia maombi yaliyowasilishwa na Vyuo na Taasisi mbalimbali kutaka nafasi zilizo wazi ziweze kujazwa. Kwa kuzingatia hilo, Baraza linatoa wito kwa wahitimu wa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita na wale wote walio na nia na sifa za kujiunga na programu mbalimbali kutumia fursa hii kutuma maombi ya udahili kwenye Taasisi na Vyuo ambavyo bado vinapokea maombi ya udahili katika ngazi ya Astashahada na Stashahada.

Aidha, Vyuo na Tasisisi zitakazohusika kwenye awamu hii, zinaarifiwa kwamba mfumo utakuwa wazi kupokea majina ya wanaodahiliwa ili kufanyiwa uhakiki hadi hiyo tarehe 10 Novemba, 2019. 

Vyuo na Taasisi zinazotaka kubadilisha taarifa za wanafunzi waliowasilishwa na kuonekana kuwa na mapungufu yaliyopelekea kukosa sifa, nazo zinashauriwa kufanya hivyo ndani ya kipindi hicho kuanzia leo tarehe 01 hadi 10 Novemba, 2019.

Ikumbukwe, kwamba uhakiki wa majina yote yatakayowasilishwa utafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 15 Novemba, 2019, na  matokeo ya uhakiki yatatolewa tarehe 17 Novemba, 2019.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.