Skip to main content

NACTE YATANGAZA AWAMU YA NNE YA UDAHILI KATIKA NGAZI YA ASTASHAHADA NA STASHAHADA KWENYE VYUO NA TAASISI MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2019/2020


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linautangazia umma kwamba limefungua dirisha la udahili kwa AWAMU YA NNE na ya mwisho, kwenye Vyuo na Taasisi zinazotoa programu za Astashahada na Stashahada hapa nchini, zinazotambuliwa na Baraza kuanzia tarehe  1 Novemba, 2019  hadi tarehe 10 Novemba, 2019 ambapo dirisha hilo litafungwa.

Hatua hiyo imekuja kufuatia maombi yaliyowasilishwa na Vyuo na Taasisi mbalimbali kutaka nafasi zilizo wazi ziweze kujazwa. Kwa kuzingatia hilo, Baraza linatoa wito kwa wahitimu wa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita na wale wote walio na nia na sifa za kujiunga na programu mbalimbali kutumia fursa hii kutuma maombi ya udahili kwenye Taasisi na Vyuo ambavyo bado vinapokea maombi ya udahili katika ngazi ya Astashahada na Stashahada.

Aidha, Vyuo na Tasisisi zitakazohusika kwenye awamu hii, zinaarifiwa kwamba mfumo utakuwa wazi kupokea majina ya wanaodahiliwa ili kufanyiwa uhakiki hadi hiyo tarehe 10 Novemba, 2019. 

Vyuo na Taasisi zinazotaka kubadilisha taarifa za wanafunzi waliowasilishwa na kuonekana kuwa na mapungufu yaliyopelekea kukosa sifa, nazo zinashauriwa kufanya hivyo ndani ya kipindi hicho kuanzia leo tarehe 01 hadi 10 Novemba, 2019.

Ikumbukwe, kwamba uhakiki wa majina yote yatakayowasilishwa utafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 15 Novemba, 2019, na  matokeo ya uhakiki yatatolewa tarehe 17 Novemba, 2019.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>