Skip to main content

KANUNI ZA UFUGAJI BORA BORA WA MBUZI


Mbuzi ni moja ya wanyama ambao wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu pia ni wavumilivu wa ukame na maradhi tofauti na ngo’mbe kwa kua wana umbile dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na nguvu kazi ndogo na hata kwa wenye kipato kidogo.

Pia mbuzi huzaa (uzao) kwa muda mfupi ili kumwezesha mfugaji kuwa na mifugo mingi kwa muda mfupi. Mbuzi wanaweza kufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi na mazao mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato.

Namna bora ya ufugaji.
Wafugwe kwenye banda bora.
Chagua kulingana na sifa zao na lengo la ufugaji (uzalishaji) nyama au maziwa.
Walishwe chakula sahihi kulingana na umri.
Kuzingatia ushauri wa mtaalamu wa mifugo hasahasa namna ya udhibiti wa magonjwa.
Kuweka kumbukumbu za uzalishaji.
Kuzalisha nyama au maziwa bora yanaokidhi mahitaji ya soko.

Sifa za zizi au banda bora la mbuzi.
Banda bora linatakiwa liwe ni lenye kuweza kuwakinga mbuzi au kondoo na mashambulizi ya wanyama wakali (hatari) na wezi.
Liwepo sehemu ambayo maji hayawezi kutuama.
Mabanda yatenganishwe kulingana na umri.
Liwe na ukubwa ambao linaweza kufanyiwa usafi.

Kama utafuga mbuzi kwa kuwafungia (shadidi) muda wote zingatia yafuatayo:-
Banda imara lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya,upepo/mvua.
Lenye hewa ya kutosha.
Liwe na sakafu ya kichanja na sehemu ya kuwekea chakula na maji.
Liwe na vyumba tofauti kwa kuweka vijitoto/wanao ugua/wanao kua.

 Ujenzi wa banda la mbuzi.
Banda lijengwe kwa kutumia vifaa vilivyopo eneo husika na kwa kuzingatia uwezo wa mfugaji.
Kuta ziwe imara na zinazo ruhusu mwanga na hewa ya kutosha.
Mlango uwe na ukubwa wa 60X150 sentimeta.
Sakafu iwe ya udongo/zege ya kichanja unaweza kutumia mabanzi/mianzi na iruhusu kinyesi na mikojo kudondoka chini.
Chumba cha majike na vitoto kiwe na sentimeta 1.25kati ya fito na fito au papi na papi, chumba cha mbuzi wakubwa kiwe na sentimeta 1.9 kati ya mbao na mbao.

Ansante kwa kuwa nasi katika makala haya ya ufugaji, usikose sehemu ya pili ya somo lijalo jinsi ya kuchagua mbegu bora ya mbuzi wa kuwafuga.


Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.