Skip to main content

TAKUKURU YAMPANDISHA KIZIMBANI MHADHIRI AKIOMBA RUSHWA YA NGONO



Oktoba 9, 2019 Takukuru imeieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jinsi ilivyomkamata mhadhiri msaidizi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Samson Mahimbo mwenye umri wa miaka 68 akiwa mtupu akimtaka kingono mwanafunzi wake Victoria Faustine kwenye nyumba ya kulala wageni.

Hayo yameelezwa na wakili wa taasisi hiyo ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini Tanzania, Faraja Salamba wakati akimsomea maelezo ya awali mshtakiwa huyo mbele ya Hakimu mkazi mkuu, Huruma Shahidi.

Amedai kuwa Januari 5 na 11, 2017 mshtakiwa alitumia madaraka yake vibaya kuomba rushwa ya ngono baada ya kumpigia simu  mwanafunzi wake Victoria Faustine na kumsisitiza wakutane katika baa ya Shani.

TMA yatoa tahadhari ya mvua kubwa kwa siku 5
Ambapo Victoria aliitikia wito kukutana na mhadhiri Samson ambaye alikuja na mtihani wa marudio wa somo alilokuwa akifundisha na majibu alimpa, alipomaliza akasahihisha na kumpa alama ya 67.

Inadaiwa kuwa mara baada ya Victoria kumaliza kufanya mtihani huo na kusahihishiwa walihamia baa nyingine ya Camp David na kunywa pombe na mshtakiwa kuchukua chumba.

Mahakama hiyo imeelezwa kuwa walipoingia chumbani mshtakiwa alivua suruali na kubaki na nguo ya ndani na kumkumbatia mwanafunzi huyo.

Salamba amesema wakati mhadhiri huyo akimvua nguo mwanafunzi huyo, mlango uligongwa na Victoria alikwenda kufungua na waliingia maofisa wa Takukuru.

Aidha moja ya Profesa amewahi kuhojiwa jina lake limehifadhiwa amesema kuwa moja ya sababu kubwa ni pale ambapo mhadhiri anapotamani kutumia nafasi yake vibaya kujinufaisha na ngono huku mwanafunzi nae akitamani kupata alama za bure mara nyingi imekuwa ikiwaponza.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.