Skip to main content

TGNP YAWAPA WANAWAKE MBINU ZA KUSHINDA UCHAGUZI



Shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Gender Networking Programme (TGNP), limetoa mafunzo ya mbinu mbalimbali za kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa kwa wanawake 64 wilayani Songwe mkoani Ruvuma kwa wenye nia ya kugombea kwa lengo la kuwajengea uwezo.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere Dar es Salaam, Henry Kigodi, amesema TGNP imejikita katika kusaidia wanawake ambao wana nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ili kuweka usawa kwa kupata viongozi wanawake ambao kwa kipindi kirefu wameshindwa kufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya kukosa mbinu za kampeni na kukabiliana na mfumo dume.

Kigodi amesema wanawake wakipata uongozi huwa makini katika kufanya maamuzi, kutekeleza na kusimamia shughuli za kimaendeleo kwa kuwa wanawake hukabiliwa zaidi na changamoto za kimaendeleo katika vitongoji, vijiji na mitaani kuliko wanaume.

"Wanawake ni watu pekee wanaohangaika na changamoto zilizopo mitaani kama vile uhaba wa maji, huduma za afya pamoja na malezi napia ni watu wenye ushiriki wa kiwango cha juu katika shughuli za uzalishaji mali kama kilimo lakini hawafaidiki na chochote,” Amesema Kigodi.

Naye mwezeshaji mwenza, Gratiana Rwakibarila, amesema wanawake wanapaswa kutambua kuwa wana uwezo mkubwa katika suala la uongozi, hivyo wanawajibu mkubwa katika kuhakikisha wanapata mbinu za ushindi kwa kupata mafunzo ili kujenga uwelewa.

Aidha, Rwakibarila amesema mafunzo hayo yatawaboreshea mbinu walizokuwa nazo za kampeni wakati wa uchaguzi, Pia ametaja vyama vinavoshiriki mafunzo hayo kuwa ni CCM, CUF, CHADEMA, TLP pamoja na ADATADEA.i

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.