Wakulima wa zao la kahawa wa kata ya Mugoma wilayani Ngara mkoani Kagera wamekatishwa tamaa na zao Hilo kutokana na kushuka bei kwakiasi kikubwa.
Wakizungumza na Muungwana Blog baadhi ya wakulima hao wamesema kuwa zao hilo limeshuka bei wakati wa uuzaji wao kwani mwaka jana kahawa Kg1 ilikuwa ikiuzwa 1800 lakini kwasasa huuzwa Kg1 1100.
Wamesema hali hiyo ya uuzaji wa kahawa inawakatisha tamaa kama wakulima kwani kahawa ndio tegemezi lao katika maisha yao ya kila siku.
Gedion ambaye ni mkulima wa zao hilo amesema kuwa kahawa imeshuka kiasi kikubwa hali ambayo inapelekea kutokujikwamua kiuchumi.
Shukuru ambaye pia ni mkulima amesema zao hilo limemewakatisha tamaa kutokana nakushuka bei mara kwa Mara wakati wa uuzaji wao kwa wafanyabiashara.
"Kama mwaka huu zao kahawa Kg1 1100 na mwaka jana ilikuwa Kg1 1800 unaona ni jinsi gani tunapata hasara wakati wa uuzaji wetu wakati tunatumia gharama kubwa wakati wakulima." Amesema Shukuru
Cosmas Bishundu ni mwenyekiti wa kitongoji cha Mkagugo kijiji cha Mruvyagira kata ya Mugoma amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo kwa wakulima hao nakuwatoa wasiwasi kwani tatizo hilo ashalifikisha kwa viongozi wa juu nalinafanyiwa kazi.

Comments
Post a Comment
Yes