Skip to main content

MAMBO YA KUYATAZAMA ILI KUONGEZA THAMANI KATIKA BIASHARA



Huenda ukawa anafanya biashara au unapenda kufanya biashara lakini yapo baadhi ya mambo ya msingi ya kuyatazama kabla  au wakati wa kufanya biashara. Tupo baadhi yetu tunashindwa kufikia malengo yetu hasa katika kuwaza au kupoifanya biashara. Leo katika makala haya nitakwenda kukueleza juu ya kujijengea misingi ili kukuza  na kuongeza uthamani wa biashara.

Biashara yeyeto ile endapo itafanya kwa misingi ambayo inafaa itakuwa na faida sana. Zipo baadhi ya biashara hazikui kwa sababu  ya kuzifanya biahara hizo miaka yote kwa staili moja. Kama kweli unataka kukuza biashara yako ni lazima utazame ni kwa jinsi gani unaweza kubadilisha mfumo wa kiutendaji ambao utakufanya uweze  kupata faida zaidi. Biashara hata kama itakuwa ndogo au kubwa kiasi gani endapo utaifanya kwa ubunifu na umakini wa hali ya juu utaongeza wateja zaidi.

Yafuatayo ndio mambo ya msingi ya kuongeza uthamani wa biashara ili kuongeza wateja zaidi;

Ladha na  fasheni.
Kimsingi kuna baadhi ya watu huwa tunafanya biashara tu bila kuangalia vitu kama  vile ladha  au fasheni (mitindo inayokwenda na wakati) . huenda ukawa haujanielewa ngoja nikupe mfano kama wewe unafanya biashara angalie wateja wako wanakula au wanakunywa kwa sababu ya kukidhi mahitaji au kwa sababu wanaridhika na kile wanachokula au kunywa. Kama wewe unafanya biashara nyingine kama vile, nguo, viatu, magari, vitu vya ujenzi vitu vingine ni lazima uangalie vitu vinavyokwenda na wakati , kwani endapo utafanya hivyo ndivo vitavyokufa uongeze wateja. Tukumbuke ya kuwa kadri vitu vinavyokuwa vya fasheni ndivo wateja wabavozidi kuwa wengi.

Kipato cha wateja.
Katika kutazama ni vipi unaweza kuongeza uthamani wa biashara jambo la msingi ni kujua kipato cha wateja wako.  Kama eneo ambalo unaishi wateja wako wanaoishi ni watu wa kipato cha kawaida ni lazima ujue ya kuwa bidhaa na bei lazima vilingane na wateja wako mfano huwezi kwenda kuanzisha biashara ya super market kijijini. Pia tukumbuke ya kuwa kuna baadhi za bidhaa endapo bei zitakuwa chini ndio huwa zinawateja wengi zaidi, halikadhalika kama wateja wako ni watu wa kipato cha juu basi bidhaa na bei ya bidhaa zako ni lazima yakidhi mahitaji ya watu hao kwa namna moja au nyingine.

Uhitaji wa bidhaa.
Katika biashara ni lazima uangalie uhitaji wa bidhaa au huduma kwa wateja wako. Kanununi za kibiashara zinasema kwamba kama kama bidhaa  zina gharama ndogo za uzaji uhitaji wa wateja hua mkubwa sana na kinyume chake inawezekana pia. Pia ni lazima usome soko lako kwa maana ya kuangalia wateja wako wanahitaji nini, na ujalibu kuchua mahitaji yao na kuwahudumia bidhaa hizo ili kukidhi mahitaji yao.

Matangazo
Matangazo husiana na jinsi ya upatikanaji na matumizi ya bidhaa au huduma husika. Ili kuwavutia wateja juu ya biashara yako ni vyema kuitangaza bidhaa yako ili kuwafanya  wateja waweze kuitambua biashara ambayo unaifanya. Katika kuitambulisha bidhaa katika matangazo ni lazima uwe mbunifu ili tangazo linapomfikia mtumiaji ahisi yeye ni sahemu ya biashara hiyo kwa maana ya kwamba mtumiaji aseme bila bidhaa hawezikuishi.

Hali ya hewa.
Biashara ni yeyote ni lazima ujue ni kipindi gani bidhaa yako itauzika zaidi. Biashara zingine ni za msimu kwa mfano kama unauza miavuli najua utaifanya kwa nguvu zaidi kipindi cha mvua. Hivyo kwa kuwa wewe ndo unataka kuifanya biashara au umekwisha kuanza biashara ni lazima uzingatie je biashara yako  itauzika zaidi msimu gan? Ukizingatia hayo, biashara yako iatakuwa ni yenye faida kubwa.

Kama unataka kufanya biashara au unafanya biashara na unataka kupata faida kubwa ni lazima uzingatie hayo kwa namna moja ama nyingine.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.