Skip to main content

FAIDA ZITOKANAZO NA ULAJI WA UGALI WA DONA



Watu wengi hupendelea ugali mweupe, au watu wengine hupenda kuuita sembe, Faida ya sembe ni vile unavyoweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu bila kuharibika kuliko dona na wapo wengine huipenda sembe labda inavutia machoni tu kutokana na rangi yake.

Ila ulaji wa dona na dona la mahindi ya njano una faida nyingi kiafya na kiuchumi!

1. Una virurutbisho muhimu vikiwemo vitamini na madini mbalimbali yanayohitajika kwa afya ya mwili na akili. Katika sembe virutubisho vyote huondokewa kwa kukoboa.

2. Una nyuzi lishe ambazo husaidia msukumo na mmeng'enyi wa chakula, hivyo huzuia matatizo ya kukosa kubwa na hata saratani ya utumbo mpana.

3. Hupunguza hatari ya kupata magonjwa yasiyiambukizwa yakiwemo kisukari, uzito kupita kiasi, shinikizo la damu n.k kwa sababu kiasi cha wanga kinachoweza kuchukuliwa huwa kidogo kwenye dona kuliko sembe.

4. Mahindi ya njano yana vitamin A kwa wingi ambayo ni muhimu kwa afya ya macho, ngozi na mifumo mbalimbali mwilini.

5. Unapunguza gharama na muda wa kukoboa na kutupa chakula kama mapumba.

Wengi tunashangaa mbona kasi ya magonjwa ni mengi kuliko zamani kumbe wachawi ni sisi wenyewe. Hebu anza leo kula ugali wa dona uone maajabu yaliyo ndani yake.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).