Skip to main content

KANUNI ZA KUNYUNYIZIA DAWA SHAMBANI


Nakukalibisha mpenzi msomaji wa blog yetu pendwa, nahuu niwakati mwingine tena wa kuendelea kujifunza mambo mengi zaidi kuhusiana na kilimo. Na leo nitakuelezea kanuni za kunyunyuzia dawa shambani.

Awali ya yote nataka kukuelezea maana ya kunyunyuzia dawa au spraying kwa lugha ya kitaalamu. kunyunyuzia(spraying) nikitendo cha kulinda mazao na wadudu na magonjwa kwa kusambaza kiasi kidogo cha viwatilifu katika mmea mama.

 Kemikali unyunyuziwa kama mchanganyiko kwa kiasi kidogo, kati au kikubwa juu ya mmea mama ili kuulinda na wadudu au ugonjwa flani kwa hali ya kimiminika.

Vifaa tofauti tofauti vya kunyunyuzia dawa/ viwatilifu
Aina tofauti tofauti ya vinyunyuzi hutumiwa kulingana na aina ya zao, kipato cha mkulimwa na ukubwa wa shamba, vifuatavyo ni vifaa hivyo.

AERIAL SPRAYER; hiki ni kifaa kinacho huusisha ndege katika kunyunyuzia, ni mahususi katika zao la viazi au mazao mengine ya mboga mboga ambayo uhitaji kutibiwa katika kipindi ambacho mataili ya trekta yanaweza kujeruhi mazao hayo.

MANUAL KNAPSACK SPRAYER; Hiki ni kifaa ambacho mnyunyuziaji hukibeba mgongoni na kutumia mkono wake mmoja kupamp na mwingine kuelekeza nozzle katika mazao, na kifaa hiki hubeba little 5 hadi 15 za dawa iliyo changanya na maji.

MOTORIZED KNAPSACK SPRAYER; Hiki ni kifaa ambacho pia kinafanana na nilicho kitaja mara ya pili, tofauti yake hiki kinakua na engine ambayo huzunguka na kuwezesha dawa kwenda umbali mrefu, kifaa hiki utumiwa mahali ambapo Manual knapsack sprayer kinakua hakina uwezo wa kufikisha mfano miti. na kifaa hiku hubeba little 15 hadi 20.

TREE SPRAYER; Hiki kifaa hutumika kunyunyuzia dawa katika miti midogo, mfano miti ya matunda.

BOOM SPRAYER; Pia kifaa hiki hutumika kunyunyuzia dawa katika mashamba makubwa sana, na hufanya kazi kwa kuambatanisha katika trekta. kifaa hiki ubeba litter tofauti tofauti mfano 4000, 6000 nakadhalika.

Kanuni za kunyunyuzia dawa.
Zifuatazo ni kanunu muhimu ambazo unatakiwa uzingatie wakati wa kunyunyuzia dawa.
angalia uelekeo wa upepo kabla ya kunyunyuzia dawa,
Nilazima uvae vifaa vya kukulinda mfano groves na mask
Hakikisha kifaa chako kimefungwa vizuri
Osha kifaa chako cha kunyunyuzia kabla na baada ya kukitumia
Tunza kifaa chako mahali safi na kavu
Changanya na koroga dawa yako vizuri kabla ya kunyunyuzia
Hakikisha unatumia vipo sahihi.

Bila shaka mpenzi msomaji umejifunza mengi zaidi katika somo hili.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.