Skip to main content

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM KUANZA KUTOA MITIHANI YA KISWAHILI YA KIMATAIFA KUANZIA JANUARI 2020


Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Katika jitihada za kukuza na kuieneza lugha ya Kiswahili,Chuo kikuu cha Dar es Salaam mapema mwezi January mwaka 2020 kinatarajia kuanza kutoa mitihani ya kimataifa ya ujuzi wa lugha hiyo.
 
Akizungumza na waandishi wa habari hii jana Jijini Dodoma,Katibu mkuu wa Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt.Leonard Akwilapo amesema kuwa katika awamu hii wameona mafanikio makubwa katika kuiendeleza
lugha ya Kiswahili kwani sasa imekuwa moja kati ya lugha rasmi za Jumuiya ya nchi za kusini mwa Afrika yaani SADC

Dkt.Akwilapo ameongeza kuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitakuwa ndio Chuo kikuu cha kwanza Duniani kutunga mitihani hiyo,kusimamia udahiri na usahihishaji wake na kutoa cheti cha kimataifa kinachoonesha kiwango cha ujuzi wa mtahiniwa ambapo pia ametabainisha walengwa wa mitihani hiyo

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtanzania kutoka Taasisi ya Confucius,Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Mgoda Mutembei yeye amesema kuwa kuna wananfunzi wengi wanaosoma lugha ya Kiswahili nje ya nchi na wangependa kutambulkika kuwa wamesoma lugha hiyo kwa kuwa na cheti
maalumu hivyo Chuo kikuu cha Dar es Salaam kitakuwa ni suluhisho katika suala hilo.

Dkt.Akwilapo pia ameuhakikishia umma kuwa tayari kuna makubaliano baina ya walimu wa Kiswahili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na walimu wanaofundisha kiswahili katika vyuo vya nje kuhusiana na mitihani hiyo

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>