Skip to main content

SERIKARI YAITAKA BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU KUTOCHELEWESHA FEDHA


 Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia William Ole Nasha ameitaka Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu HESLB kutochelewesha fedha za mikopo kwa wanufaika 

Akizungumza jijini Dar es salaam Ole Nasha amesema serikali imeshataoa fedha kwa Bodi ya Mikopo kiasi cha shilingi Bilioni 125 ili kuwezesha utoaji mikopo hiyo.

 "Bodi ya Mikopo pamoja na kuendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi hakikisheni wanafunzi 5,593 ambao taarifa zao zilikua na matatizo zinashughulikiwa kwa haraka kwa kufungua dirisha dogo la maombi ili nao wapate haki yao ya msingi," amesisitiza Naibu Waziri Ole Nasha.

Aidha naibu waziri huyo amepiga marufuku kwa wanafunzi wa vyuo vikuu wanaopata mkopo wa shilingi milioni 2 na laki nne kwa mwaka kwa ajili ya malazi na chakula kuacha kuita mkopo huo kuwa ni mkopo ziro.

"Kuanzia leo tunapiga marufuku matumizi ya neno 'Mkopo Zero' , haiwezekani Serikali yao ijitahidi kuwatafutia fedha ya mkopo kwa ajili ya maradhi na Chakula halafu useme Mkopo Sifuri, ni marufuku kutumia msamiati huo"- Amesema Naibu Waziri, William Ole Nasha

Naye Mkurugenzi Mtendaji Bodi ya mikopo HESLB Abdul-Razaq Badru amesema baadhi ya wanafunzi wanafanya makosa wakati wa uombaji hali ambayo inawakwamisha kupata mikopo kwa wakati.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Taasisi za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu TAHLISO Alex Stephano ameiomba bodi hiyo kutatua changamoto ambazo bado zinazowakabili wanafunzi wa vyuo vikuu wakati wa kujaza fomu hizo za maombi.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.