Skip to main content

HII NDIO MISEMO ITAKAYOKUPA MOTISHA YA KUFANIKIWA ZAIDI




Mafanikio ya maana tofauti kati ya mtu na mtu. Wengine wanaamini kwamba watakuwa wmefanikiwa wakiweza kuwa na pesa ya kiasi fulani. Ila kwa wengine, kuishi vizuri na kusaidia watu kupitia kazi yao ndio kufanikiwa.  Kama tulivvyo sema mwanzoni, maana ya kufanikiwa inatofautiana kati mtu na mtu. Ila, watu wenye mafanikio huwa wana sifa zinazofanana.

Miongoni mwa sifa zinazofanana kwa watu waliofanikiwa ni pamoja na kujituma. Mtu aliyefanikiwa ni mtu anayeongea kwa matendo na sio maneno.

Ila, kwa kuwa inaweza ikachukua muda kuwa na sifa zote hizo, tumia misemo 10 ifuatayo kukuongezea motisha:

1. “Nafasi za kufanikiwa hazijitokezi hivi hivi, inabidi uzitengeneze” – Chris Grosser

2. “Njia pekee ya kufanya kazi nzuri ni kupenda kazi yako. Kama hujapata kazi unayoipenda, endelea kuitafuta. Usiridhike” – Steve Jobs

3. “Mtu asiyewahi kukosea hajawahi kujaribu kitu kipya” – Albert Einstein

4. “Kama kila kitu kingekuwa kimekamilika, usinge jifunza chochote na usingekuwa” – Beyonce Knowles

5. “Ndoto ni kitu nzuri. Ila, ni ndoto tu. Ndoto hazifanikiwa kuwa kweli kwa kuwa umeziota. Kuchapa kazi ndio inafanya ufanikiwe. Kuchapa kazi ndio kinachosabibisha mabadiliko” – Shonda Rhimes

6. “Labda hautashindwa kama mimi nilivyoshindwa, ila, mara nyingine kushindwa hakuepukiki. Haiwezekani kuishi bila kushindwa kufanya kitu mara moja, labda uwe unaishi kwa tahadhari kwa kiasi kikubwa kwamba bora usingeishi kabisa – na hapo, tayari utakuwa umeshindwa” – J.K Rowling

7. “Simjui mtu yoyote aliyewahi kufika ngazi za juu bila kuchapa kazi. Hiyo ndiyo kichocheo. Na labda haitakufikisha juu kabisa, ila utakaribia” – Margaret Thatcher

8. “Kufanikiwa kwa kishindo, inabidi ujaribu kufanya vitu vikubwa” – Bill Gates

9. “Bora uwe na marafiki waliokuzidi. Chagua marafiki wenye tabia nzuri kuliko ya kwako na utaishia kuwafuata” – Warren Buffet

10. “Tunaweza tukashindwa mara nyingi, ila tusikubali kushindwa kabisa kabisa” – Maya Angelou

Misemo yote haya yana ujumbe zinazofanana. Tegemea kushindwa, chapa kazi, chagua kazi unayoipenda na jihusishe na watu watakao kuongezea  motisha na kukusukuma ili ufanikiwe.

Wote hawa walikuwa na mapambano yao binafsi ila hawakuruhusu kushindwa mara kwa mara iwakatishe tamaa. Na wewe pia inabidi ufanye hivyo. Kumbuka, chochote kile unachopitia kita pita.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.