Skip to main content

TAEC YATOA MAFUNZO UKAGUZI WA MIZIGO BANDARINI



Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), Profesa Lazaro Busagala amewataka watumishi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kuhakikisha wanafanyia kazi mafunzo waliyoyapata ya ukaguzi wa mizigo kwa njia ya teknolojia ya Nyuklia kwa lengo la kuongeza ufanisi bandarini hapo.

Mafunzo hayo ya wiki mbili ya ukaguzi wa mizigo kwa kutumia teknolojia ya Nyuklia yametolewa kwa wafanyakazi 22 wa Kitengo cha Midaki (scanner) katika Bandari ya Dar es Salaam ambapo yamelenga kuwapa uwezo wafanyakazi wanaoshugulikia ukaguzi wa mizigo katika midaki (Scanner) katika eneo la Bandari kwa lengo kuongeza kasi na weledi katika ufanyaji kazi kwa lengo la kuharakisha ukaguzi wa mizigo Bandarini.

“Hakikisheni mnatumia mafunzo haya katika kufanya kazi kwa weledi na kuongeza tija ili kusiwe na ucheleweshwaji wa mizigo hapa bandarini,” amesema Profesa Busagala.

Pamoja na mambo mengine, Profesa Busagala amesema TAEC itaendelea na jukumu lake la kutoa mafunzo ili kuhakikisha usalama katika maeneo yote yenye vyanzo vya mionzi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha  Midaki (Sscanner) Bandarini, Mtani Rugina amesema  wataendelea kuhakikisha wafanyakazi wote waliopo kwenye maeneo ya ukaguzi wa mizigo bandarini hapo wanapata mafunzo ili kuboresha ufanisi katika ufanyaji kazi wao.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>