Skip to main content

LAINI ZA SIMU ZISIZOSAJILIWA KWA ALAMA ZA VIDOLE KUZIMWA IFIKAPO DESEMBA 30


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kanda ya ziwa kwa kushirikiana na mamlaka ya vitambulisho NIDA pamoja na watoa huduma za mawasiliano ya simu wameanzisha kampeni maalumu ya kufanya usajili wa laini za simu kwa njia za vidole.

Kampeni hiyo inatarajiwa kuanza Septemba 30, 2019, mkoani Mwanza eneo la Rock City Mall ambapo itenda kwa jina la mimi nimesajili namba yangu ya simu wewe unangoja nini?, kampeni hiyo inatarajiwa kufanywa kwa kipindi chote hadi pale zoezi la usajili litakapositishwa mnamo Disemba 31, 2019.

Akizungumza leo Septemba 27, 2019 Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano, Mhandisi Francis Mihayo, amewaomba wananchi kuhakikisha wanafanya zoezi hilo mapema ili kuondokana na usumbufu utakaojitokeza mwishoni mwa zoezi hilo.

Amesema ambao hawatasajili laini zao hadi ifikapo Disemba 31, 2019, zitasitishwa kutoa huduma zote ikiwa pamoja na kupiga na kupokea simu.

Aidha, Afisa wa NIDA, Raphael Manase amesema kuwa watakwepo katika usajili huo ambapo wameongeza wigo mpana zaidi kwa mwananchi kuweza kujua namba zao za usajili wa vitambulisho vyao vya taifa kulingana na mahali walipo.

Ambapo ametoa hatua kuu tatu ambazo mtu anaweza kutumia ili kuweza kupata namba yake ya usajili kama alishasajiliwa awali

”Hatua ya kwanza unayoweza kufanya kupata namba yako ya usajili wa kitambulisho cha Taifa ni kwenda Serikali ya Mitaa, au serikali ya vijiji namba zimeenda kwa uongozi wa serikali za mitaa na serikali za kijiji’, mbili unaweza kupata hizo namba kwa njia ya simu kwa kupiga *152*00# au kutembelea tovuti yetu ya NIDA ambayo unaweza kuinga pale kwa kuandika www.nida.go.tz kuna sehemu imeandikwa kitambulisho cha taifa, kuna option mbili kwanza kujua namba ya kitambulisho pili kupata kopi ya kitambulisho ambapo kuna maswali utaulizwa ili kuthibitishwa” amesema Manase

Ameongezea kuwa Kwa wale ambao bado hawajasailiwa wanasahuriwa kufika ofisi za NIDA ili kusaidiwa zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>