Skip to main content

FAIDA ZA LIMAO AU NDIMU KILISHE NA AFYA




Zifuatazo ndizo faida zitokanazo na utumiaji wa limao na ndimu kilishe na kiafya;
Kusaidia uwiano sahihi wa pH ya mwili kuuwezesha kufanya shughuli mbalimbali.

Ina vitamin C na kemikali mimea ambayo husaidia kutibu mafua na mfumo wa upumuaji. Pia kuboresha afya ya ngozi, fizi (kuzuia fizi kutoka damu, ukavu wa ngozi ikiwemo kuchanika midomi na pua kavu), moyo, figo, misuli, maini na ubongo kwa kupambana na sumu mbalimbali mwilini. Pia husaidia kukata uchovu wa mazoezi au marathon.

Husaidia mfumo wa mmeng'enyo wa chakula, kunywa sharubati yenye mchanganyiko wa limao au ndimu, au bilauli ya maji ya limao au ndimu nusu saa kabla ya kula.

Pia tindikali zilizonazo husaidia kuzuia au kupambana na vijiwe vya figo, gout (mlundiknoi wa uric acid kwenye viungo na mwili). Husaidia kufyonzwa na kubadilisha madini ya chuma kwenye vyakula jamii ya mimea na kufanya iweze kutumika kutengeneza damu (ferrous iron).

Ganda la limao pia lina virutubisho, kemikali mimea na mafuta kwa wingi. Ganda lake au mafuta husaidia kutibu mafua, kuchua misuli au hutumika kwenye vinywaji kuleta ladha au kama tiba mvuke kwa magonjwa ya msongo wa mawazo, au magonjwa ya mifumo ya fahamu.

Matumizi ya mara kwa mara Husaidia kupambana na kisukari, shinikizo la damu (kutokana na wingi wa potassium) na ulemavu wa macho.

Matumizi ya kila siku kwa muda mrefu Husaidia kuzuia saratani mbalimbali mwilini.
Husaidia mchakato wa kuzalisha nguvu mwilini.

 Mambo muhimu ya kuzingatia.
Inashauriwa kuongeza limao/ndimu kwenye mboga za majani kama tembele na chai ili kusaidia ufyonzwaji na utumiwaji wa madini ya chuma mwilini toka kwenye mboga hizo.

Faida hizi pia zafanana na jamii zote za malimao yakiwemo machungwa, madalansi, machenza nk japo baadhi ya faida zinaweza kuwa kwa wingi au kidogo kwa kila tunda

Inashauriwa kutumia moja ya matunda hayo kila siku ili kuboresha lishe na afya zetu.

Angalizo
Wapo wanaotumia limao kuondoa kichefuchefu au kuzuia kutapika, ila limao halizuii kutapika, bali inapelekea kutapika kutokana na uchachu wake. Hivyo waweza tumia parachichi au tunda baridi (lisilo chachu) kuzuia kutapika.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.