Skip to main content

TANZANIA KUTEKELEZA MPANGO MKAKATI WA MAENDELEO KWA NCHI WANACHAMA WA UMOJA WA AFRIKA (AU)


Farida Ramadhani na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Tanzania imejipanga kutekeleza Mpango Mkakati wa Maendeleo kwa nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kwa lengo kuchochea maendeleo endelevu nchini na kupunguza umaskini kwa wananchi wake.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Adolf Ndunguru, wakati wa warsha ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika kuhusu Uasilishaji wa Agenda 2063 ya Maendeleo ya Afrika.

Bw. Ndunguru ameeleza kuwa, Tanzania imejipanga kutengeneza mazingira yatakayowezesha kutekeleza mpango huo nchini kwa kuhakikisha unaingia katika mipango ya maendeleo ya nchi ili kuchochea maendeleo ya huduma za afya, utoaji wa elimu, maendeleo ya viwanda pamoja na ukuaji wa uchumi wa nchi.

Alisema maendelo sio kwa ajili ya watu wachache hivyo Serikali imejipanga kushirikisha wananchi wote katika kutekeleza mpango mkakati huo kwa kuhakikisha wanaelewa chanzo cha mpango huo pamoja na manufaa yake nchini.

“Tumeamua kuuleta mkakati huu nyumbani ili kuhakikisha kwamba Watanzania wanajua Agenda 2063 ya maendeleo na umuhimu wake kwao, kila mtanzania ajione ni sehemu ya mpango huo na hakuna atakayeachwa nyuma”, alisisitiza Bw. Ndunguru.

Akizungumzia Mpango Mkakati huo, Kamishna Msaidizi wa Sera kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Wiliam Mhoja, alisema kuwa Agenda 2063 ni Mpango Mkakati wa Maendeleo ya AU, ambao umejiwekea malengo takribani 20 kuhusu ukuaji wa uchumi jumuishi pamoja na maendeleo endelevu.

Alisema kuwa miongoni mwa malengo hayo ni pamoja na kuboresha miundombinu ya usafiri kama reli na barabara ambayo itaunganisha nchi zote za Afrika.

Bw. Mhoja alisema kuwa mpango huo utaanza kuwekwa katika mpango wa maendeleo ya nchi pamoja na kuwajengea wananchi uelewa ikizingatiwa kuwa Taifa lipo katika uandaaji wa mpango wa tatu wa maendeleo.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi wa Sera kutoka Kamisheni ya AU, Bw. Oitsile Thesunyiwe, alisema kuwa Kamisheni hiyo imekuwa ikijenga uelewa wa kuhusu Agenda 2063 kwa nchi Wanachama wa umoja huo ambapo Tanzania ni nchi ya 43 kutembelewa kati ya nchi takribani 55 katika umoja huo.

Alisema katika kutoa uelewa wa agenda hiyo, Kamisheni ya Umoja wa Afrika inafanya mazungumzo na nchi hizo kuhusu namna ya kuhuisha Agenda 2063 katika mipango ya maendeleo ya Taifa na ya kisekta.


Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.