Skip to main content

MPANGO KAZI WA TAIFA WA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO WAJADILIWA


NA.MWANDISHI WETU
WADAU wa masuala ya Wanawake na Watoto wamekutana ili kujadili na kufanya tathimini ya Utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) kwa kipindi cha robo ya kwanza 2019/2020.

Akizungumza wakati akifungua kikao kazi hicho cha siku mbili kuanzia Septemba 18 hadi 19, 2019 kilichofanyika katika Ukumbi wa Bwalo la JKT UMWEMA mkoani Morogoro Mratibu wa Taifa wa Mpango huo Bi. Happiness Mugyabuso amesema, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo wameandaa kikao kazi hicho ili kujadili na kufanya tathimini ya utekelezaji wa Mpango Kazi huo.

 “Leo tumekutana hapa kwa pamoja kwa lengo la kufanya tathimini ya utekelezaji wa mpango kazi huo katika kipindi cha robo ya kwanza kwa Mwaka 2019/2020. Aliongezea kuwa, pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika robo ya kwanza ya utekelezaji wa Mpango Kazi, kikao kazi kitajadili pia changamoto zilizojitokeza katika kipindi husika na kuweka mikakati mahsusi ya kuimarisha utekelezaji wake kwa vipindi vya robo zinazofuata,”alisema Bi. Happiness.

Aidha kikao hicho kilitoa fursa ya kujadili namna bora ya kuboresha mfumo wa ukusanyaji na uchakataji wa taarifa za takwimu za utekelezaji wa MTAKUWWA ili kuimarisha upatikanaji wa takwimu za msingi (baseline data). Hatua hii ni muhimu kwani itasaidia kupima hali ya utekelezaji wa Mpango Kazi katika vipindi mbalimbali vikiwemo vya mwaka na miaka mitano (5).

Mmoja wa washiriki wa kikao hicho Bw.Emmanuel Burton ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii alieleza kuwa, Miongoni mwa maeneo yaliyojadiliwa ni pamoja na namna bora ya upatikanaji wa taarifa sahihi za utekelezaji katika sekta mbalimbali ambazo zinatekeleza mpango huo na kuwa na mikakati ya namna ya kuwafikia walengwa kikamilifu ili kukidhi lengo mpango ifikapo mwaka 2021/ 2022.

“Kikao kazi hiki ni muhimu kwa kuzingatia kuwa, malengo mahsusi ya utekelezaji wa Mpango wa MTAKUWWA yanajadiliwa na kuhakikisha tunaandaa taarifa sahihi zenye tija kuhusu makundi hayo ili vita dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto inapiganwa na kuleta matokeo chanya,”alisema Burton

=MWISHO=

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.