Skip to main content

WAZIRI WA FEDHA AWASIMAMISHA KAZI MAAFISA MANUNUZI WA TAASISI 6



Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango ameagiza kusimamishwa kazi maofisa ununuzi wa Veta, ASA, NIMR, kituo cha Diplomasia na halmashauri ya Wilaya Kaliua na Nsimbo kupisha uchuguzi kufuatia ripoti ya PPRA kuonyesha uzingatiaji hafifu wa sheria ya manunuzi ya umma katika taasisi zao huku akiwataka viongozi wa Taasisi hizo kujipima kama wanatosha katika nafasi zao.

Ametoa maagizo hayo jana akipokea ripoti ya tathmini ya utendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa mwaka 2018/19 iliyoonesha kuwa kulikuwa na udhaifu wa uzingatiaji wa sheria za manunuzi ya Umma katika Taasisi hizo

Maafisa ununuzi hao ni kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Wakala wa Mbuga za Kilimo, Taasisi ya Utafiti wa Dawa (NIMR), Kituo cha Diplomasia, Halmashauri ya Kaliua na Nsibo

Aidha, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi na kuchukua hatua kwa Taasisi zote ambazo miradi yake haina thamani ya fedha na ile ambayo ripoti inaonesha ilikuwa na viashiria vya rushwa

Miradi ambayo haina thamani halisi ya fedha ni pamoja na mradi wa uchimbaji wa mashimo ya kuchakata taka ngumu wa Halmashauri ya Kahama na usambazaji wa mita za maji katika Halmashauri hiyo hiyo

Baadhi ya Taasisi ambazo miradi yake ilikuwa na viashiria vya rushwa ni Wizara ya Maji, Shirika la Reli Tanzania (TRC), Shirika la viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya majisafi na majitaka, Singida na Wanging’ombe na Manispaa za Kigamboni, Ubungo na Kahama

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.