Skip to main content

NCHI 60 KUSHIRIKI MAONYESHO YA UTALII TANZANIA


 Zikiwa zimebaki siku 57 kufikia Tamasha kubwa la utalii hapa Nchini linalofahamika kama “Swahili International Tourism Expo” , Bodi ya utalii Tanzania TTB imethibitisha kuwa imejipanga vema kuwapokea wageni toka nchi 60 watakaoshiriki Tamasha hilo. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari  Jijini Dar es Salaam leo , Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii, Devotha Mdachi  ameeleza kuwa Tamasha hilo litafanyika  oktoba 18 hadi 20 mwaka huu, katika Kumbi za Mikutano Mlimani City, huku  mawakala zaidi ya 200 wakitarajiwa kushiriki katika Maonyesho hayo. 

Hata hivyo, Devotha amesema juhudi za kufanikisha ujio wa wageni hao zaidi ya 200 kutoka Nchi 60 zimefanywa kwa ushirikiano mkubwa kutoka Bodi ya Utalii TTB pamoja na Balozi zetu mbalimbali za nje. 

“mpaka sasa tumepokea uthibitisho kutoka ofisi za ubalozi; toka nchi mbalimbali zikiwemo Ubalozi wa Sweden, Ubalozi wa Tanzania Nchini Malaysia,  Ubalozi wa Tanzania Nchini China, Ubalozi wa Korea ya Kusini,  Ubalozi wa Japani, Ubalozi wa Kanada, Ubalozi wa Afrika Kusini, Ubalozi wa Omani, Ubalozi wa India,  Ubalozi wa Uingereza,  Ubalozi wa Brazili” Amezita Mkurugenzi Devotha 

Akieleza zaidi juu ya upokeaji wa wageni hao watakaofika katika Tamasha hilo, amesema wamejipanga  na kujiboresha zaidi kwa  kuwapeleka katika maeneo mbalimbali ya utalii nchini, ikiwemo  Hifadhi ya Wanyama Serengeti, Uduzungwa, Mikumi,  Fukwe za Tanga, Mapango ya Amboni, Mlima Kilimanjaro, Miradi ya Utalii wa Utamaduni mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, pia visiwa vya Zanzibar na Mafia. 

Sambamba na hilo, kampuni na Mashirika mbalimbali  zaidi ya 30 yamejitolea kuunga mkono juhudi hizo zinazofanywa na TTB katika kuelekea kilele cha Maonesho hayo. 

“kampuni kuu ambazo tayari zimetoa udhamini ni  The Global Vector Control Standard, Benki ya CRDB ambayo ni mdau mkubwa  katika sekta ya Utalii … pamoja na shirika la Ndege la Ethiopia” 

Mkurugenzi alitaja wadhamini wetu wakiwemo ni Air Tanzania … Hifadhi ya Taifa TANAPA, Mamlaka ya Hifadhi ya NgoroNgoro, Mamlaka ya Wanyama Pori Tower, Wakala wa Misitu TFS, na vyama vya Utalii.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.