Skip to main content

KWA MARA YA KWANZA WANASAYANSI WAGUNDUA MAJI KWENYE SAYARI YA MBALI



Kwa mara ya kwanza wataalamu wa anga wamegundua maji katika sayari inayozunguka katika nyota iliyoko orbiti yenye mazingira sawa na yaliyo duniani.

Utambuzi huo unaifanya dunia inayotambulika kwa lugha za kisayansi K2-18b kua ni moja ya sehemu zitakazofanyiwa utafiti juu ya viumbe wanaoaminika kuwepo duniani 'aliens'.

Ndani ya miaka kumi kuanzia sasa, darubini mpya ina uwezo wa kutambua kama anga za sayari K2-18b ina gesi ambazo zina uwezekano kua zilitokana na viumbe hai.

Taarifa hizo zimeandikwa na jarida la kisayansi la 'Nature Astronomy'.


Prof. Giovanna Tinnetti, mwanasayansi aliyeongoza watafiti kutokea chuo cha London (UCL),ameeleza kuwa ugunduzi huo ni mkubwa.

"Hii ni mara ya kwanza kwa maji kugunduliwa kwenye sayari yenye hali sawa na dunia, katika nyota hii ambayo hali ya hewa yake ni rafiki kwa maisha ya viumbe hai"Profesa alifafanua.

Sayari hii mpya ina ukubwa mara mbili ya dunia na katika kundi lake inajulikana kama "Super Earth" na ina hali ya hewa inayoweza kuruhusu maji au kimiminika kuanzia nyuzi joto sifuri mpaka.

Sayari ya K2-18b yenye umbali wa maili millioni 650 kutoka duniani ni miaka 111 kwa spidi ya mwanga, hivyo ni ngumu kutuma kifaa huko

Hivyo nafasi pekee ya kuitambua zaidi ni kusubiri kwa kizazi kijacho cha wana anga kuitambua zaidi sayari hiyo hasa kwa darubini mpya itakayozinduliwa kuanzia miaka ya 2020.

Timu ya wanasayansi iliyogundua ilipitia sayari zilizogunduliwa na Hubble Space Telescope kati ya mwaka 2016 na 2017 na ndipo walipoigundua K2-18b kuwa ina uwezo wa kuwa na maji.

Wana-anga wengine wanapingana na taarifa hiyo juu ya uwezekano wa viumbe wengine kuishi.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.