Skip to main content

SERIKALI YATUMIA MIRADI KUDHIBITI UHARIBIFU WA MAZINGIRA


Serikali imechukua hatua mbalimbali kupitia miradi inayofadhiliwa na Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi ili kuweza kudhibiti uharibifu wa mazingira unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi katika Visiwa vya Pemba na Unguja.

Hayo yamesemwa leo Septemba 5,2019 na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima akiwa Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Mwantum Dau Haji lililouliza kuwa kasi ya mmomonyoko wa ardhi na uhaba wa udongo katika Visiwa vya Unguja na Pemba vinatishia uhai wa visiwa hivyo. Je, ni hatua zipi za makusudi zimechukuliwa katika kuvinusuru visiwa hivyo?. 

Mhe. Sima alisema kupitia Mradi wa Kujenga Uwezo wa Jamii Kuhimili Athari za Mabadiliko ya tabianchi-LDCF ambao umetekelezwa mwaka 2012 hadi 2018, shughuli mbalimbali zimefanyika zikiwemo ujenzi wa kuta mbili za mita 25 kila moja katika eneo la Kisiwa Panza-Pemba na ujenzi wa makinga bahari (groynes) matano ya wastani wa urefu wa mita 100 kila moja katika eneo la urefu wa mita 538 Kilimani-Unguja. 

Pia Naibu Waziri alitaja upandaji mikoko Pemba maeneo ya Kisiwa Panza hekta 200, Tumbe hekta 10, Ukele hekta 7 na Tovuni hekta 1 na upandaji mikoko Unguja maeneo ya Kisakasaka hekta 8 na Kilimani hekta 1.4. 

Aliongeza kuwa kupitia mradi wa Kupunguza Uharibifu wa Ardhi na Kuongeza Uzalishaji wa Chakula katika maeneo kame nchini (2017-2022), shughuli zinazotegemewa kufanyika katika maeneo ya Micheweni Kata ya Micheweni na Kiuyu Maziwang’ombe ambazo ni kujenga makinga maji katika mashamba (dykes) ili kuzuia maji ya bahari kuingia katika mashamba. 

Nyingine ni kutoa elimu kuhusu kilimo kinachokabiliana na mabadiliko ya tabianchi kupitia mashamba darasa, upandaji  wa miti ili kuhifadhi udongo na kutunza mazingira, na uanzishaji wa biashara ndogo ndogo ili kuwezesha jamii kuwa na shughuli mbadala za kujiongezea kipato.  


Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi, kudhibiti mmomonyoko wa udongo, na kukabiliana na uhaba wa udongo. Alimalizia Waziri Sima.
 

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>