Skip to main content

BRELA WATOA MAFUNZO KUHUSU UTOAJI WA LESENI ZA BIASHARA.



Kufuatia kauli mbiu ya Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Pombe Magufuli inayosema Tanzania ya uchumi wa viwanda wakala wa usajili wa leseni za biashara na makampuni  “BRELA”  wametoa mafunzo kuhusu utoaji wa leseni za biashara kwa mfumo wa kielektroniki “NATIONAL BUSINESS PORTAL” katika halmashauri ya Manispaa ya Bukoba  Mkoani Kagera.

Nae Afisa Biashara kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw. Denis Mzamiru amefafanua kuhusu mfumo huo kuwa ni moja ya jitihada za awamu ya tano ili kuwawekea urahisi wa mazingira ya biashara kwa wafanya biashara ya ndani na nje.

“Kama mnavyojua Tanzania ni nchi ya kibiashara pia hata sisi tumeona mfumo huu utarahisisha taaraifa za mfanyabiashara hata hivyo tunalazimika kuweka taarifa za biashara katika mtandao vilevile tumepunguza changamoto kwa wafanya biashara kuacha kwenda umbali mrefu hili kupata lesseni pia itapunguza mianya yaa rushwa kupitia mifumo hii pamoja na kupanua wigo wa serikali katika kupata mapato zaidi”

Hata hivyo,  Ndg. Merkisedek Kalinga kwa niaba ya Afisa biashara wa mkoa ambae pia ni mchumi amewasisitiza wafanya biashara walioudhuria mafunzo hayo kuwa mfumo huu utawasaidi zaidi hata katika upatikanaji wa taarifa zao katika kupitia mfumo huo mda wowote na pia itakuwa rahisi kupata leseni kwa haraka kuliko kukaa kusubili leseni wakati huo biashara ya mfanyabiashara imesimama.

Vilevile mafunzo hayo yamewashirikisha wadau mbalimbali wa biashara na makampuni wakiwemo wadau wa Bank ya NMB ambao wao ndio watu ambao leseni za wafanya biashara zinapita mikono yao wakati wakiwa wanalipia biashara zao.

Aidha nae mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba yalipo fanyika mafunzo hayo Mh. Limbe Molis ametoa wito kwa wafanya biashara kuchangamkia fursa hiyo kwa kusajili biashara zao na kukata leseni kwa mfumo wa kielektroniki “NATIONAL BUSINESS PORTAL”huku akiwashukuru wakala wa  leseni BRELA kwa kutoa mafunzo ambapo itachangia kukuza pato la mkoa pia.

Sambamba na hayo naobaadhi ya wafanya biashara  mkoani humo wameupokea vizuri mfumo huo huku wakioji na kuwataka wakala wa BRELA kutoa elimu zaidi ili kuwapa uelewa mpana wafanya biashara na wamiliki wa makampuni mbalimbali hili kuongeza pato la taifa ikiwa mafunzo ya mfumo huo yanatolewa katika wilaya sita nchi nzima.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.

NAFASI 37 ZA KAZI TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) DEADLINE 29/11/2019

The Tanzania Institute of Accountancy (TIA) is an Executive Agency under the Ministry of Finance and Planning which was established on 1st July, 2002 by the Government Notice No. 489 of 1st November, 2001 and officially launched on 24th January, 2002 as per Act No. 30 of 1997. As an Executive Agency, TIA is operating ‘semi’ autonomously and commercially in providing quality education in the field of Accountancy, Procurement & Supplies and other Business related disciplines so as to become a self-sustainable Institute. TIA is accredited by NACTE as an Institute of Higher Learning Education. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>> The Institute is looking for qualified and dedicated personnel to fill the post of Tutorial Assistants on contract basis. The table below provides details on a particular fields/ professionals one should apply against. ==>>Kujua Namna Ya Kutuma Maombi ; << Ingia Ha>>