Halmashauri ya wilaya ya Momba mkoani Songwe inakumbwa na changamoto ya mitandao ya simu muda mrefu jambo ambalo limeonekana kuwa ni kikwazo kwa wanafunzi wa chuo cha Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Slaam (DIT) Kampasi ya Myunga Momba kujifunza na kwendana na kasi ya maendeleo ya teknolijia Duniani.
Chuo cha Taasisi ya Teknolojia ya Dareslaam (DIT) Kampus ya Myunga ni chuo cha kwanza cha serikali mkoani Songwe ambacho kinategemewa kutatua changamoto mbali za ukosefu wa watalaam upande wa ufundi sanifu, sayansi na uhandisi katika fani mbalimbali.
wadau wanafunzi pamoja na wameilezea changamoto hiyo ya mawasiliano katika hafla ya awamu ya kwanza ya mafunzo ya udereva yaliyoendeshwa na chuo cha VETA Mbeya wakishirikiana na DIT Kampasi ya Myunga .
Dk Frenk Lujaji Mkurugenzi wa Chuo cha DIT Kampasi ya Miyunga alisema kuwa mtandao ni muhimu sana kwa chuo hicho kwa kuwa kimejikita zaidi katika ufundi ambao unaendana sambamba na teknolia ambayo inakua kila siku kutokana na maendeleo ya Sayansi Duniani kwa ujumla.
"Sisi kama chuo baada ya kuona chanagamoto hii ni kubwa tuliamua kuwasiliana na TTCL ambapo wanaendelea kutuboreshea ili tuweze kwendana na teknolojia, kila kitu unacho fanya katika teknolojia lazima ufanye ulinganifu na sehemu zingine Duniani, hivyo kupatikana kwa mtandao wa uhakika kutaboresha mawasiliano na kuboresha mafunzo kwa wanafunzi ili kwendana na Soko la ajira na kujiajir" alisema Dk Lujaji.
Aliongeza kuwa lengo la chuo hicho ni kuukwamua mkoa wa Songwe kiuchumi, kwa kuzalisha mafundi na watalaam mbalimbali wano hitajika katika soko la ajira .
Adam Zakaria Kinyekile Injinia wa mitaani ambaye anatengeza ajira kwa mafundi mbalimbali kutoka vyuo vikuu nchini kutokana na ubunifu na uzopefu wake katika fani hiyo alisema kuwa katika ufundi mitandao ya simu na Internet ni muhimu sana ili kuweza kutengeneza vitu vyenye ubora kulingana na soko la Dunia linavo hitaji'
Pia ameitaka serikali kuwatambua mafundi wa mitaani walio na vipaji na uzoefu mkubwa katika fani hiyo ili waweze kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiserikali kama wazawa.
"Mitaani tupo mafundi wazuri sana ambapo tukitumiwa na serikali bila kujali kuanagalia cheti twaweza kunufaika na kunufaisha nchi yetu , mimi wanafunzi wengi kutoka vyuo vikuu huja kufanya mazoezi kwa vitendo kwangu na nmefundisha watu wengi sana ambao tayari walishajiajiri na kupunguza tatizo la ajira kwa vijana" alisema Kinyekile.
Godfrey Siame Diwani wa Kata ya Ikana eneo kilipo chuo hicho alisema changamoto ya mitandao ni changamoto kwa wananchi wake hata eneo zima la wilaya ya Momba jambo ambalo hupelekea mawasiliano kuwa magumu na kukwamisha baadhi ya shughuli muhimu hata za Kiserikali.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Songwe John Palingo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ghafla hiyo alisema kuwa tayar mkoa umesha orodhesha maeneo yote ndani ya mkoa ambayo yanachangamoto mitandao ili kufanyiwa kazi na wizara husika.
"Hii changamoto ya mitandao itaisha mwaka huu wa fedha kwa sababu tayari tumeshaainisha maeneo yote na tayari kwa kukupeleka Tamisemi ili kufanyiwa kazi kufanyiwa kazi " alisema Palingo.
Aidha Palingo alikitaka chuo hicho kujikita kutoa elimu iliyo bora na yenye ushindani ili kushindana na nchi ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo nchi 16 zilizo kusini mwa Afrika (SADC)
"Ajira zitakuwa wazi kwa nchi zote wanachama hivyo tutotoe elimu bora yenye kukidhi mahitaji ya nchi za jumuiya ya Afrika mashariki na nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo nchi 16 zilizo kusini mwa Afrika (SADC), tuanzishe programu za uzalishaji bidhaa kwenye kilimo ambazo uhitaji wake ni mkubwa" alisema Palingo.
Comments
Post a Comment
Yes