Skip to main content

WAZIRI KUWACHUKULIA HATUA WANAOTOA MIMBA



Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile, amesema  Serikali itahakikisha inakomesha uuzaji holela wa dawa mbalimbali,  hususani zile zinazotengenezwa kwa ajili ya matumizi mazuri na kugeuzwa kuwa ni za kutolea mimba.

Waziri Ndugulile ameyabainisha hayo leo Agosti 29,  baada ya Kamati ya Bajeti ya Bunge la Baraza la wawakilishi Zanzibar,  kutembelea Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Nchini Yaani (TMDA).

"Hizi dawa zinazoitwa Misoprostol ni dawa ambazo zinatumika katika uzazi kuongeza uchungu na kupunguza uvujaji wa damu,  lakini dawa hizi hizi katika matumizi yake mabaya zinaonekana zinaweza kusaidia kutoa ujauzito na hilo sasa hivi limeonekana kuwa ndiyo tumizi kuu kuliko lile tumizi la kwanza, lengo na kusudio la dawa lilikuwa ni zuri lakini sasa ni tofauti kwahiyo wajibu wetu kama Serikali ni kusimamia vizuri ". Amesema Dkt Ndugulile.

Aidha Serikali imesema itawachukulia hatua kali zaidi,  wauzaji wote  wanaouza dawa bila kutumia cheti cha daktari na kwamba serikali itaanzisha msako mkali.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUWA MWANDISHI MZURI WA VITABU

Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu  zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji. Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga. Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine. 2. Pangilia kabla ya kuandika Mpangilio ni...

HEKA HEKA VIWANJANI;KIKOSI CHA TIMU YA HR\MKT WAFANIKIWA PENYA NUSU FAINALI BAADA YA KUWACHAPA MECHANICS KATIKA VIWANJA VYA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT).

Hiki ndicho kikosi cha timu ya HR\MKT kilicho wachabanga MECHANICS Kwa goli moja bila katika kipindi cha kwanza goli lilofungwa na mchezaji mahiri maarufu kama (Jay) mwenye jezi nambari 17 mgongoni ni James Philimon akiwa na magoli matano katika michuano ya interclass na hadi kipenga cha mwisho muamuzi wa mchezo huo kumaliza mchezo na kuwafanya HR\MKT chukua point tatu muhimu mbele ya washika spana MECHANICS na kujikusanyia point tisa(9) na kufanikiwa kuingia nusu fainali Matokeo yakiwa HR\MKT 1 na MECHANICS O Hichi ndicho kikosi cha MECHANICS kilicho shindwa kutamba mbele ya timu ya mafisa waajiri wakiungana na mafisa masoko na kufanikiwa kuwatoa katika michuano ya interclass inayoendelea katika chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT).

CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI TANZANIA (NIT) KINACHO TOA MAFUNZO MBALI MBALI YA USAFIRISHAJI KINAHAKIKISHA SETKA YA UCHUKUZI INAKUWA IMARA SIKU BAADA YA SIKU.